Friday, June 14, 2013

DR. KAMALA NCHINI UHOLANZI

 Mandhari ya mji wa Rotterdam.
 Hii ni Roboti inayokamua Ng'ombe maziwa. Ng'ombe mwingine anaonekana akisubiri zamu yake.
Balozi wa Tanzania Jumuiya ya Ulaya akimuangalia Ng'ombe wa maziwa. Ng'ombe huyu anatoa lita za maziwa Mia moja kila siku. Balozi Kamala na Mabalozi wengine wa Afirka wako kwenye ziara ya mafunzo Uholanzi.
Mabalozi wa Afrika katika Nchi ya Uholanzi wakisiliza mada kuhusu bandari ya Uholanzi. Wa kwanza Kulia ni Dr. Diodorus Buberwa Kamala, Balozi wa Tanzania Jumuiya ya Ulaya.

MAZISHI YA MZEE JULIAN KIBINDO LUKINDO BABA MZAZI WA SUZANI MUNGY WA SHRIKA LA UTANGAZAJI TANZANIA TBC YA FANYIKA KIJINI KWAKE MUHEZA TANGA



Suzana Mungy wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) akiweka udongo katika kaburi la Baba yake mzazi Mzee Julian Kibindo Lukindo(78) ambaye amezikwa  jana jioni kijijini kwake Muheza Tanga Mzee Lukindo amezaliwa 1935 na amefariki tarehe 10 june2013.

RAIS KIKWETE APOKEA UJUMBA TOKA BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA


Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akipokea ujumbe maalumu toka kwa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt Donald Kaberuka ulioletwa kwake na mwakilishi mkazi wa Benki hiyo nchini Mhe Tonia Kandiero leo Juni 13, 2013 katika Ikulu Ndogo Dodoma

Wednesday, June 12, 2013

WAZIRI MKUU PINDA, DODOMA


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta na bunge wa Viti Maalum na Mkuu wa mkoa wa Rukwa, Mhandisi Stella Manyanya kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Juni12, 2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta na wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Southern Highlands yaMafinga Iringa waliotembelea Bunge Juni 12,2013.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Tuesday, June 11, 2013

WADAU WA SEKTA YA UVUVI WAWEKA MIKAKATI YA KUIMARISHA UVUVI BORA NA ENDELEVU MKOANI KAGERA


Wadau wa Sekta ya Uvuvi mkoani Kagera wakutana na kuweka mikakati mbalimbali ya kuendeleza uvuvi mkoani hapa kwa kuwanufaisha wanakagera na kuzingatia njia bora za uvuvi.
Kikao hicho kilikuwa na lengo la kujadili jinsi ya   kuuendeleza uvuvi bora katika mkoa wa Kagera aidha kubani changamoto zilizopo katika sekta hiyo na jinsi ya kuzitatua ili kuwepo na uvuvi wenye tija.
Wajumbe wa kikao hicho walijadiliana hasa jinsi ya kuendelea kutatua changamoto za bei ya samaki kati ya wavuvi na wawekezaji (wamiliki wa viwanda vya Kagera Fish na VicFish)  katika sekta hiyo ili kuinua maisha ya mvuvi wa mkoa Kagera.
Wawekezaji walishauriwa kupanga bei zao na wavuvi kwa makubaliano ambapo hawatatakiwa kuvunja makubaliano hayo  bila kuwasiliana tena na wateja wao ambao ni wavuvi ili kila mmoja ardhie bei husika.
Mkuu wa Mkoa wa Kagera mabaye aliwakilishwa na Katibu Tawala Msaidi Utawala  Bw. Richard Kwitega aliwasistiza wajumbe katika hotuba yake kuendelea na mikakati ya kupambana na uvuvi haramu, utoroshaji wa mazao  ya samaki pia kupambana na wavuvi wanaovua samaki wachanga.
Pia alisistiza sana juu ya uchafuzi wa mazingira miaroni ambako samaki wanafikia baada ya kuvuliwa ziwani. Mhe. Massawe aliwaasa na kuwakumbusha viongozi wa Halmashauri husika kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.
Kwa upande mwingine katika kikao hicho wajumbe waliweza kupata elimu juu ya “MAPANKI” masalia ya samaki baada ya kuondolewa minofu jinsi yanavyotengenezwa kama kitoweo na chakula cha mifugo na kutoa ajira kwa vijana  pia kusafirishwa nchi za nje na kupata fedha za kigeni.
Angalizo, wajumbe wa kikao hicho walitoa angalizo juu ya viongozi wa kisiasa kutoingilia utendaji wa watendaji wa serikali katika kufanya kazi zao pale wanaposimamia sheria mfano uvuvi haramu na uchafuzi wa mazingira miaroni.
Imeandaliwa na:
Sylvester Raphael
AFISA HABARI
RS-KAGERA@2013

MLIPUKO WA UGONJWA WA MALARIA ULIVYOITESA WILAYA YA MULEBA

  Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Zipporah Lyoni Pangani na Mkuu wa Wilaya Muleba Pamoja na Wataalam wa Afya Wakigawa Vyandarua Mara Baada ya Kuwaelimisha Wananchi Juu ya Nia Bora za Kuikinga na Mlipuko wa Malari Wilayani Muleba Kwenye  Mkutano wa Hadhara Katika Kata ya Kasharunga.