Mandhari ya mji wa Rotterdam.
Hii ni Roboti inayokamua Ng'ombe maziwa. Ng'ombe mwingine anaonekana akisubiri zamu yake.
Balozi wa Tanzania Jumuiya ya Ulaya akimuangalia Ng'ombe wa maziwa.
Ng'ombe huyu anatoa lita za maziwa Mia moja kila siku. Balozi Kamala na
Mabalozi wengine wa Afirka wako kwenye ziara ya mafunzo Uholanzi.
Mabalozi wa Afrika katika Nchi ya Uholanzi wakisiliza mada kuhusu
bandari ya Uholanzi. Wa kwanza Kulia ni Dr. Diodorus Buberwa Kamala,
Balozi wa Tanzania Jumuiya ya Ulaya.
Friday, June 14, 2013
MAZISHI YA MZEE JULIAN KIBINDO LUKINDO BABA MZAZI WA SUZANI MUNGY WA SHRIKA LA UTANGAZAJI TANZANIA TBC YA FANYIKA KIJINI KWAKE MUHEZA TANGA
Suzana Mungy wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) akiweka udongo katika kaburi la Baba yake mzazi Mzee Julian Kibindo Lukindo(78) ambaye amezikwa jana jioni kijijini kwake Muheza Tanga Mzee Lukindo amezaliwa 1935 na amefariki tarehe 10 june2013.
RAIS KIKWETE APOKEA UJUMBA TOKA BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA
Wednesday, June 12, 2013
WAZIRI MKUU PINDA, DODOMA
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta na bunge wa Viti Maalum na Mkuu wa mkoa wa Rukwa, Mhandisi Stella Manyanya kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Juni12, 2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta na wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Southern Highlands yaMafinga Iringa waliotembelea Bunge Juni 12,2013.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Tuesday, June 11, 2013
WADAU WA SEKTA YA UVUVI WAWEKA MIKAKATI YA KUIMARISHA UVUVI BORA NA ENDELEVU MKOANI KAGERA
Wadau
wa Sekta ya Uvuvi mkoani Kagera wakutana na kuweka mikakati mbalimbali ya
kuendeleza uvuvi mkoani hapa kwa kuwanufaisha wanakagera na kuzingatia njia
bora za uvuvi.
Kikao
hicho kilikuwa na lengo la kujadili jinsi ya
kuuendeleza uvuvi bora katika
mkoa wa Kagera aidha kubani changamoto zilizopo katika sekta hiyo na jinsi ya
kuzitatua ili kuwepo na uvuvi wenye tija.
Wajumbe
wa kikao hicho walijadiliana hasa jinsi ya kuendelea kutatua changamoto za bei
ya samaki kati ya wavuvi na wawekezaji (wamiliki wa viwanda vya Kagera Fish na
VicFish) katika sekta hiyo ili kuinua
maisha ya mvuvi wa mkoa Kagera.
Wawekezaji
walishauriwa kupanga bei zao na wavuvi kwa makubaliano ambapo hawatatakiwa
kuvunja makubaliano hayo bila
kuwasiliana tena na wateja wao ambao ni wavuvi ili kila mmoja ardhie bei
husika.
Mkuu
wa Mkoa wa Kagera mabaye aliwakilishwa na Katibu Tawala Msaidi Utawala Bw. Richard Kwitega aliwasistiza wajumbe katika
hotuba yake kuendelea na mikakati ya kupambana na uvuvi haramu, utoroshaji wa
mazao ya samaki pia kupambana na wavuvi
wanaovua samaki wachanga.
Pia
alisistiza sana juu ya uchafuzi wa mazingira miaroni ambako samaki wanafikia
baada ya kuvuliwa ziwani. Mhe. Massawe aliwaasa na kuwakumbusha viongozi wa
Halmashauri husika kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.
Kwa
upande mwingine katika kikao hicho wajumbe waliweza kupata elimu juu ya
“MAPANKI” masalia ya samaki baada ya kuondolewa minofu jinsi yanavyotengenezwa
kama kitoweo na chakula cha mifugo na kutoa ajira kwa vijana pia kusafirishwa nchi za nje na kupata fedha
za kigeni.
Angalizo,
wajumbe wa kikao hicho walitoa angalizo juu ya viongozi wa kisiasa kutoingilia
utendaji wa watendaji wa serikali katika kufanya kazi zao pale wanaposimamia
sheria mfano uvuvi haramu na uchafuzi wa mazingira miaroni.
Imeandaliwa
na:
Sylvester Raphael
AFISA HABARI
RS-KAGERA@2013
MLIPUKO WA UGONJWA WA MALARIA ULIVYOITESA WILAYA YA MULEBA
Kaimu
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Zipporah Lyoni Pangani na Mkuu wa Wilaya
Muleba Pamoja na Wataalam wa Afya Wakigawa Vyandarua Mara Baada ya
Kuwaelimisha Wananchi Juu ya Nia Bora za Kuikinga na Mlipuko wa Malari
Wilayani Muleba Kwenye Mkutano wa Hadhara Katika Kata ya Kasharunga.
Subscribe to:
Posts (Atom)
