Tuesday, December 16, 2014

JESHI LA POLISI KAGERA LATAWANYA MAANDAMANO YA WAFUASI WA CHADEMA


Jeshi la polisi mkoani KAGERA limelazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wafuasi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)  waliofanya maandamamo yasiyokuwa na kibali  kufuatia ushindi mkubwa ambao chama hicho kimeupata katika manispaa ya BUKOBA.

Maandamamo hayo yalikuwa yameanzia  katika kata ya KASHAI kubwa kuliko zote katika manispaa ya BUKOBA ambayo chama hicho  kimeshinda mitaa yote TISA yalikuwa yakielekea kwenye uwanja wa michezo wa KAITABA.

Kufutia hatua ya jeshi la polisi ya kuzuia maandamano hayo, JUSTINIAN EVODIUS, katibu wa baraza la vijana la CHADEMA anaeleza namna jeshi la polisi ambavyo halikuwatendea na jambo lililowapelekea wanachama wa chama hicho kuandamana,  naye HENRY MWAIBAMBE ni kamanda wa jeshi la polisi mkoani KAGERA anayetoa onyo kwa  yoyote atakayefanya maamdamano bila kibali.

INSERT No.1…….Justinian Evodius…..katibu wa baraza la vijana CHADEMA
INSERT No.2……Henry Mwaibambe….kamanda wa jeshi la polisi Kagera

Kwa upande wake, VICTOR SHEREJEY katibu wa  CHADEMA katika manispaa ya BUKOBA anaeleza mikakati ya chama hicho na mambo yaliyopelekea kisishinde mitaa yote, nao  MATELU ANDREA, IGNUS KAMBUGA na BAKARI IBRAHIMU ni miongoni  wananchi katika manispaa ya BUKOBA wanaokitahadhalisha  Chama Cha Mapinduzi (CCM)  huku wakielezea hali ya uchaguzi.

INSERT No.3…Victor Sherejey….katibu CHADEMA Bukoba
INSERT No4……Matelu Andrea……mwananchi
INSERT No.5……Ignus Kambuga…….mwananchi
INSERT No.6……Bakari Ibrahimu…..mwananchi

Katika uchaguzi wa serikali za mitaa katika manispaa ya BUKOBA, CHADEMA imeshinda mitaa ISHIRINI na TISA katika uchaguzi uliopita chama hicho kilipata mitaa TISA, katika uchaguzi huu CCM imeshinda mitaa THERATHINI na TANO na Chama cha wananchi  (CUF) kimeshinda viti VIWILI.

No comments:

Post a Comment