Friday, December 19, 2014

SERIKALI YANUSURU MAISHA YA WALIOTAKA KUSAFIRI NA MELI YA MV VICTORIA

Baadhi ya wafanyabiashara waliokuwa  wamepakia mizigo yao ndani meli ya MV VICTORIA  iliyotarajiwa jana kuondoka  bandari ya  BUKOBA  kuelekea bandari ya  MWANZA wameandamana hadi ofisi ya mkuu wa wilaya ya BUKOBA kupinga hatua ya mamlaka ya uthibiti wa usafiri wa maji na nchi kavu (SUMATRA) ya kuzuia safari ya meli hiyo  isiendelee na safari.
Mamlaka hiyo imefikia uamzi wa kuzuia safari hiyo  baada ya kubaini matatizo ya kiufundi ya meli hiyo,  imedaiwa meli  hiyo iliyotoka  bandari ya MWANZA siku ya jumanne  na kufika bandari ya BUKOBA jumatano majira ya saa MOJA na NUSU asubuhi kuwa ilisafiri kwa kutumia  injini moja hali ambayo ni hatari kwa usalama wa abiria na mizigo.

Kufuatia hatua ya  SUMATRA ya  ya kuzuia safari ya meli hiyo baadhi ya wafanyabiashara  hasa waliokuwa wamepakia mizigo inayoharibika haraka ambayo ni pamoja na ndizi mbivu , maparachichi  na mazao mengine hapa wanalalamika kwa kuiomba serikali iwanusuru kwa kuiruhusu meli hiyo iendelee na safari ili waweze kuokoa sehemu bidhaa zao ambazo zimeanza kuharibika.



 ZIPORAH PANGANI ambaye ni mkuu wa wilaya ya BUKOBA  anaongea na wafanyabiashara waliofanya mgomo na kuwaeleza namna serikali itakavyotatua tatizo hilo, ALEX KATAMA ni Meneja wa SUMATRA ambaye anaeleza sababu za mamlaka hiyo kuzuia meli hiyo, naye MATHEW BAJUMUZI  afisa wa shirika la huduma za meli anaeleza kilichijitokeza, huku  JOHN MONGELLAakisisitiza kwamba serikali ya mkoa wa KAGERA haitaruhusu meli hiyo hadi ijiridhishe kwa lengo la kulinda usalama wa abiria na mali zao.


Meli hiyo inasadikiwa kuwa ni mbovu na inataka matengenezo makubwa, katika kipindi cha miezi MITATU imezimika mara TANO ikiwa ndani ya ziwa VICTORIA wakati ikiendelea n a safari zake.


No comments:

Post a Comment