Thursday, December 11, 2014

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI



Katibu Mkuu wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) Ndugu Sixtus Mapunda anategemea kufanya ziara ya siku na nne (14) katika mikoa minne ya Kanda ya Ziwa, ambayo ni Tabora, Shinyanga, Geita na Kagera kuanzia kesho tarehe 12st Dec 2014.

Ziara hii ya kikazi ya Katibu Mkuu inalenga kukagua na kuhimiza ujenzi na uimara wa jumuia ya Vijana katika maeneo husika lakini pia kushiriki kampeni zinazoendelea za uchaguzi wa Serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mnamo tarehe 14th Dec 2014.

Pia, Katibu Mkuu anatarajia kufanya mikutano ya ndani na viongozi wa Jumuiya na Chama, pia kufanya mikutano ya hadhara inayolenga kuingiza wanachama wapya ndani ya jumuiya na chama kwa ujumla.

Kuhimiza wanachama wa chama cha mapinduzi na viongozi kuwaandaa wananchi katika kuipigia kura katiba mpya iliyopendekezwa wakati ukifika.

Ziara hiyo ya Katibu Mkuu inategemea kumalizika tarehe 25th Dec 2014.

Kidumu Chama Cha Mapinduzi.

No comments:

Post a Comment