Sunday, March 15, 2015

VITENDO VYA MAUAJI YA WATU VYAENDELEA KUKITHIRI KATIKA KATA YA KITENDAGURO



NA AUDAX MUTIGANZI
BUKOBA

Vitendo  vya  mauaji  vinavyofanywa na watu  wasiojulikana katika kata ya KITENDAGURO iliyoko katika  halmashauri ya manispaa ya BUKOBA wavimeendelea kukithiri , kukithiri kwa vitendo hivyo kunafuatia  kuuawa kwa watu wengine wawili kwa nyakati tofauti  katika maeneo ya  kata hiyo waliokatwa kukatwa katwa na mapanga  kichwani.

Akizungumza na waandishi wa habari kamanda wa jeshi la polisi mkoani KAGERA, kamishina msaidizi wa jeshi hilo, HENRY MWAIBAMBE  amewataja  watu  waliuwawa kuwa ni pamoja  na EMANI  DILIDI aliyekuwa akiiishi katika mkazi wa mtaa wa KANAZI na EVALIST MALISELI aliyekuwa akiishi mtaa wa KAGEMU.

Kufuatia kwa mauaji hayo MWAIBAMBE amesema jeshi la polisi mkoani KAGERA linawashikilia watu KUMI na WAWILI kwa tuhuma ya kuhusika na mauaji hayo, amewaomba wananchi kulipa ushirikiano keshi hilo ili liweze kuwabainiwanaojihusisha na matukio hayo ya mauaji pamojana kueleza kwamba jeshi  hilo kwamba linayafanyia uchunguzi wa kina matukio hayo.

Vitendo vya  mauaji ya watu katika kata ya KITENDAGULO  iliyoko katika manispaa ya BUKOBA vilianza  tangu mwaka jana, hadi sasa  zaidi ya watu KUMI wameishauwawa  kwa kukatwa katwa na mapanga na watu wasiojulikana, mauaji hayo yamewajenga hofu kubwa wananchi katika kata hiyo hadi kufikia hatua ya kutotembea wakati wa usiku.













No comments:

Post a Comment